Mwendesha mashtaka wa serikali katika kesi ya Kukwepa kodi
inayomkabili Lionel Messi na baba yake Jorge, amemshauri hakimu wa
mahakama ya Hispania kumuachia huru mwanasoka bora wa dunia.
Katika
taarifa yake rasmi aliyoitoa leo hii, mwendesha mashtaka huyo amesema
kwamba hakukuwa na jaribio lolote la Messi kukwepa kodi na hivyo
amemshauri hakimu kumuachia huru nahodha huyo wa Argentina. Hata hivyo,
mashtaka dhidi ya baba ya mchezaji huyo, Jorge Messi, yataendelea
kusimama na mwendesha mashtaka ameshauri aadhibiwe kwenda jela kwa miezi
18.

Kwa
upande wa mwanasheria wa serikali wmeendelea kusisitiza kwamba Lionel
Messi alikuwa anafahamu kuhusu makampuni yaliyotengenezwa katika kukwepa
kodi. Wanataka Messi na baba yake wapigwe nyundo ya miezi 22 kila
mmoja.

Baada
ya kumalizika kusikilizwa kwa kesi, Messi amesafiri kuelekea Marekani
kuungana na timu yake ya taifa kwa ajili ya michuano ya Copa America.
No comments